TSHISHIMBI ATOA UFAFANUZI SUALA LA KUTAKA KUONDOKA YANGA
Nahodha wa Yanga raia wa Congo DR Papy Kabamba Tshishimbi ameeleza ukweli kuhusiana na kinachoenea mitandaoni kuwa anamaliza mkataba wake na yuko mbioni kuondoka Yanga kitu ambacho amekitolea ufafanuzi lakini amegoma kueleza moja kama anabaki au.
“Mitandaoni wanachanganya sana, siwezi kusema nimeshamalizana na Yanga sababu nina mkataba na Yanga hata kama wa mwezi mmoja ni mkataba, ikitokea Yanga hainitaki nina maamuzi yangu nitaendelea kuwatumikia” alisema Tshishimbi katika mahojiano na Clouds TV
Papy Kabamba Tshishimbi ni miongoni mwa wachezaji wa Yanga wanaomaliza mikataba yao mwisho wa msiku wa 2019/20 na inawezekana akaondoka sababu ya kuanza kuhusishwa kutakiwa na vilabu mbalimbali.