SIMBA SC NGOMA INOGILE, STAND WAMECHEMKA MIKWAJU YA PENATI
Simba leo ilikuwa mkoani Shinyanga kukipiga dhidi ya Stand United katika mchezo wa Kombe la Azam Sports Federation (ASFC) uwanja wa Kambarage Shinyanga.
Mchezo ulikuwa mgumu kwa Simba tofauti na matarajio ya wengi na kujikuta Simba SC wakimaliza mchezo kwa sare ya kufungana 1-1, bao lao likipatikana kwa penati dakika ya 52 la Stand likifungwa dakika ya 67 na Miraj Salehe.
Mikwaju ya penati ndio ikaimaliza Stand na kujikuta wakiiaga ASFC kwa kushinda penati 2 tu kati ya 5 wakati Simba wakishinda penati 3 kati ya 5 na kutinga robo fainali ya ASFC kwa ushindi wa penati 3-2.