Arsenal yavunja rekodi ya Usajili
Klabu ya Arsenal imefikia makubaliano na klabu ya Lille juu ya usajili wa winga Nicolas Pepe utakaogharimu kiasi cha Pauni milioni 72.
Kiasi hicho cha fedha za usajili wa mchezaji huyo wa Ivory Coast kitalipwa kwa awamu kutokana na na bajeti yao ya usajili katika majira ya kiangazi kuwazuia.
Usajili huo unataraji kukamilika ndani ya saa 24 mpaka 48 zijazo.
Mchezaji huyo mwenye miaka 24 alifunga magoli 23 na kutoa assist 13 katika mechi 41 za Lille alizocheza msimu uliopita.