Rasmi, N’golo Kante amwaga wino Chelsea
Kiungo N’golo Kante amesaini mkataba mpya wa miaka mitano katika klabu ya Chelsea utakaomfanya aitumikie timu hiyo mpaka mwaka 2023.
Kante alikuwa akihusishwa na kujiunga na PSG majira ya kiangazi baada ya kuonesha kiwango kizuri akiwa na France kwenye michuano ya kombe la dunia nchini Russia
Mchezaji huyo anaendelea kubaki Chelsea baada ya kuwa mchezaji muhimu kwa kikosi cha Maurizo Sarri baada ya Antonio Conte kuondoka.