SCHALKE 04 WAPIGWA FAINI KWA UBAGUZI WA RANGI
Klabu ya Schalke 04 imepigwa faini ya euro 50,000 (Tsh milioni 126) kwa mashabiki wao kuimba nyimbo za kibaguzi katika mechi ya German Cup dhidi ya Hertha Berlin, chama cha soka cha Ujerumani kimetangaza (DFB) jana Jumanne.
Mchezaji wa Hertha Berlin Jordan Torunarigha alisema kuwa ndiye aliyelengwa mara kadhaa na mashabiki hao wa Schalke katika mechi hiyo ya hatua ya 16 bora iliyopigwa Februari 04.
DFB wamesema mchezaji huyo alifanyiwa ubaguzi wa rangi dakika ya 85 na kundi la mashabiki wa timu ya nyumbani,Schalke
“Kulikuwa na kelele za nyani zilifanywa.” – Walisema DFB katika taarifa yao waliyotoa.
Schalke walifanikiwa kushinda mechi hiyo kwa goli 3-2 na kufuzu hatua ya robo fainali ambapo watakutana na Bayern Munich.