JOSE MOURINHO AMPIGA CHINI VICTOR WANYAMA
Kocha wa Tottenham Jose Mourinho amemuondoa kiungo Mkenya Victor Wanyama katika kikosi chake cha klabu bingwa Ulaya msimu huu na nafasi yake kuchukuliwa na kipa Michael Vorm.
Kocha huyo amesema amemtoa Wanyama kutokana na nafasi yake anayocheza kuwepo na wachezaji wengi kama vile Harry Winks,Eric Dier,Gedson Fernandes,Oliver Skipp.
Danny Rose ambaye yupo kwa mkopo Newcastle United na Christian Eriksen ambaye amesajiliwa Inter Milan,nafasi zao katika kikosi hicho cha klabu bingwa zimechukuliwa na Steven Bergwijn na Gedson Fernandes ambao wamesajiliwa katika dirisha dogo la usajili lililopita mwezi Januari.