ANDRE GOMES ARUHUSIWA KUTOKA HOSPITALINI BAADA YA UPASUAJI
Kiungo wa Everton Andre Gomes, ameruhusiwa kutoka hospitali baada ya kufanyiwa upasuaji wa kifundo cha mguu.
Kiungo huyu aliumia katika mechi iliyoisha kwa sare ya 1 – 1 dhidi ya Tottenham Jumapili iliyopita.
Gomes sasa ataendelea kuwa chini ya uangalizi wa madaktari wa klabu, huku taarifa toka klabu hiyo ikisema upasuaji ulienda vyema na mchezaji huyo anatarajia kupona kwa ukamilifu.
Kwa upande wa Son Heung Min, kadi yake nyekundu aliyoipata kutokana na tukio hilo imefutwa na FA baada ya klabu yake ya Tottenham kukata rufaa.