Jopo la madaktari limethibitisha Messi kawafata Inter Milan
Tarifa iliyothibitisha kusafiri kwa Messi ilieleza kuwa “Mchezaji huyu atasafiri na tayari jopo la madaktari limeshajiridhisha, anaweza kuwa sehemu ya kikosi kitakachopambana dhidi ya Inter Milan keshokutwa jumatano”.
Messi alikosa mchezo wa mkondo wa tatu wa ligi ya mabingwa barani Ulaya dhidi ya Inter Milan uliomalizika kwa FC Barcelona kuibuka na ushindi wa mabao mawili kwa sifuri, kisha akaendelea kuwa nje ya kikosi kwenye mchezo wa ligi ya Hispania uliowakutanisha na Real Madrid waliokubali bakora 5 kwa 1.
Messi alirejea mazoezini juma lililopita, lakini hakucheza mchezo wa jumamosi dhidi ya Rayo Vallecano ambao walifungwa mabao matatu kwa mawili.
FC Barcelona wanaongoza msimamo wa kundi B, baada ya kushinda michezo mitatu, huku wapinzani wao Inter Milan wakishika nafasi ya pili kwa kushinda michezo miwiwli na kupoteza mmoja.