Italia wamkumbuka Davide Astori
Mechi zote za Serie A wikiendi hii iliyopita zilisimama katika dakika ya 13 kumkumbuka nahodha wa zamani wa Fiorentina Davide Astori ambaye ametimiza mwaka tangu afariki dunia.
Beki huyo ambaye alifariki Machi 04,2018 akiwa na miaka 31, alikuwa akivaa jezi namba 13 katika maisha yake ya soka.

Astori alifariki akiwa usingizini Hotelini mjini Udine huko Italia ambapo Fiorentina ilienda kucheza na Udinese, baadae ilitajwa kuwa kifo chake kilisababishwa na matatizo ya moyo.

Katika kumuenzi Muitalia huyo, Fiorentina ilistaafisha jezi namba 13 na pia waliupa uwanja wao wa mazoezi jina lake.